
Lee Daniel anakabiliwa na kesi nyingine kutoka kwa mtu ambae anasema wazo la filamu ya “Empire” lilikuwa wazo lake kwanza, ripoti zinaeleza mtoto wa Marvin Gaye III ni mtu wa mwisho kusema Lee Daniel aliiba wazo lake.
Gaye III anasema kwamba alisajili show hiyo inayohusu familia ya African-American katika kiwanda cha muziki kwa Writers Guild of America mwaka 2010.Empire imekuwa hit series, Mpango wa kesi hiyo kwa Gaye III ni kuwashtaki FOX, Lee Daniel na wengine waliohusika.
Daniel amekuwa akifunguliwa kesi mbalimbali, siku si nyingi, mwanamke mmoja wa Michigan alisema yeye ndiyo Cookie Lyon wa kweli na aliyetengeneza show hiyo aliiba stori kwenye autobiography ambayo ilionyeshwa mwaka 2010. Mwanamke huyo Sophia Eggleston anamshtaki mtengenezaji wa Empire anataka alipwe dola milioni 300.
