
Mtuhumiwa Omar Yusuf Makame
Hakimu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Isaac Sepetu, ameagiza mtuhumiwa Omar Yusuf Makame wa mauaji ya Padre Evaristus Mushi afikishwe mahakamani mara moja siku ya Jumatatu wiki ijayo, ikiwa ni pamoja na nyaraka zinazoeleza ni kwa nini hakupandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka ndani ya saa 24 kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 390 cha mwenendo wa makosa ya jinai, sura na. 7 ya mwaka 2004. Maombi ya kufikishwa mahaknani yametoka kwenye jopo la mawakili watetezi wa mtuhumiwa.
