
Mkali wa ngoma wa Started from the bottom Drake repa kutoka Toronto Canada amejiita yeye na J.Cole ndo wafalme wawili tu katika gemu la rap dunainia, na Kendrick akaungana na Cole kwa ajili ya show yake ya “Dolla & A Dream” huko Los Angeles Marekani.
Ilikuwa Julai 23 wakati J.Cole akiwa kwenye tour ya “Dollar & A Dream” LA California ambap alitokea Drake na Kendrick Lamar, wakati Drake akiperform repa huyo kutoka lebo ya YMCMB aliripotiwa akisema “Hawa ndo wafalme wawili katika rap game kwa sasa akiwa kwenye stage yani yeye na J.cole ilirpotiwa na BoomBox na baada ya hapo mtangazaji wa redio anaefahamika kama Teddy Mora kupitia twitter account yake alitweet hivi:
“Drake got on Stage, grabbed J. Cole & said “These are the ONLY 2 KINGS in the game right now on stage”.. In LA !! Thoughts ? #Kendrick ?”
Redio ya Los Angeles ya Power 106 mtangazaji Rikki Martinez alipost video ya Drake akisema hayo kwamba “Kuna wafalme wawili tu kwa sasa, wamesimama kwenye stage hii”
J.cole aliperform show mbili siku hiyo Los Angeles The Belasco, Drake alitokea wakati wa show ya kwanza wakti Kendrick aliperform kwenye show ya pili.
